Taarifa
ikufikie kwamba aliekua daktari wa mwimbaji staa wa Pop duniani Michael
Jackson, Conrad Murray ameachiwa huru kutoka jela baada ya kutumikia
kifungo kwa miaka miwili kati ya minne aliyokua amehukumiwa kutokana na
kifo cha MJ mwaka 2009.
CNN wameripoti kwamba Daktari huyu ilibidi atumie mlango mwingine kutoka jela ili kukwepa waandishi wa habari pamoja na baadhi ya mashabiki wa Michael Jackson wenye hasira waliokuwemo nje ya jela baada ya kupata taarifa kwamba anatolewa kwenye jela hiyo ya Los Angeles.
Mwanasheria wake amekaririwa akisema kwamba Doctor Conrad anaweza kurudi kuendelea na kazi yake ya udaktari lakini moja kati ya kauli za familia ya Michael Jackson ni ‘ni wazi kwamba Conrad ndio alimuua Michael Jackson, tunamatumaini kwamba hatofanya udaktari tena na kumuumiza wengine’
CNN wameripoti kwamba Daktari huyu ilibidi atumie mlango mwingine kutoka jela ili kukwepa waandishi wa habari pamoja na baadhi ya mashabiki wa Michael Jackson wenye hasira waliokuwemo nje ya jela baada ya kupata taarifa kwamba anatolewa kwenye jela hiyo ya Los Angeles.
Mwanasheria wake amekaririwa akisema kwamba Doctor Conrad anaweza kurudi kuendelea na kazi yake ya udaktari lakini moja kati ya kauli za familia ya Michael Jackson ni ‘ni wazi kwamba Conrad ndio alimuua Michael Jackson, tunamatumaini kwamba hatofanya udaktari tena na kumuumiza wengine’