![]() |
| Baada ya tuzo za KTMA kumalizika kila mmoja amekuwa na mtazamo
wake,Wiki hii Producer wa wimbo wa ‘Number One’ wa Diamond, Sheddy
Clever alitoa malalamiko yake ya kukosa tuzo ya mtayarishaji bora huku
wimbo alioutengeneza ukimpa Diamond zaidi ya tuzo tano. Producer mkongwe Joachim Kimaryo aka Master J ametoa mtazamo wake kuhusu Tuzo za KTMA 2014 ambao unaonesha hakuridhishwa na mshindi wa tuzo ya mtayarishaji bora wa mwaka – kizazi kipya ambaye ni Man Water wa Combinenga. “Sijaelewa damond kupata tuzo 7 alafu produza wake kutoka na 0!!!!!” ni jibu la moja ya maswali kuhusiana na tuzo hizo aliyokutana nayo Master J Jana alipokuwa mgeni katika session ya ‘Kikaangoni Live’ kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV. |

