![]() |
Rais wa Marekani Barrack Obama atatoa heshima zake za kutambua mateso ya
utumwa na ukomavu wa kidemokrasia nchini Senegal licha ya kuwa katika
eneo linalokumbwa na misukosuko katika ziara yake ya pili barani Afrika.
Rais Obama aliwasili katika mji mkuu wa Senegal, Dakar, jana usiku
anakoanzia ziara ya nchi tatu za Afrika ikiwemo Afrika kusini na
Tanzania katika jitihada za utawala wake kuyatimiza matarajio ya bara
hilo ambalo ndilo chimbuko la asili yake.Anaandamana na mkewe Michelle Obama na binti zake wawili Sasha na Malia na ziara yake hiyo imegubikwa kwa kiasi fulani na hali ya afya ya shujaa wa Afrika Nelson Mandela ambayo inazidi kuzorota akiwa amelazwa katika hospitali mjini Pretoria na kutishia kuvuruga ratiba ya Obama nchini Afrika ya Kusini. |
Habari kubwa Magazetini Kenya leo March 3, 2025
8 months ago

