Sonko |
Pamoja na Usharobaro wake,
Gideon Mbuvi maarufu kama Sonko… yule mbunge aliependwa na wengi na
anaejichanganya sana na watu wa kipato cha chini ametangazwa mshindi wa
kiti cha Useneta wa Jiji la Nairobi Kenya ambapo alitoa machozi kwa
kutoamini kama kweli ameshinda.
Hiyo picha hapo chini japo
haionekani vizuri inamuonyesha Sonko wakati akitangazwa mshindi, alikua
kapiga T shirt yake ya njano, kofia na hereni pia kama kawaida… alafu
kwenye mkono akatupia pete kadhaa za gold pamoja na saa kubwa mkono wa
kushoto.
Sonko ambae amepata umaarufu
kwa Usharobaro wake pia ambao ulimfanya kuwa Mbunge wa kwanza kwenye
historia ya Kenya kuingia bungeni amevaa hereni, ameshinda kwa kupata
kura zaidi ya laki nane wakati mpinzani wake Wanjiru aliepata kura laki
tano.
Sonko ni mtu wa kujichanganya
sana, nakumbuka hata wakati ule Z Anto wa Binti kiziwi yuko juu kwenye
chati, Sonko alimpatia usafiri pamoja na walinzi wa kutembea nae wakati
alipoalikwa kwenye kupafom Kenya.
Akijielezea baada ya Matokeo |