Godfrey Nyange |
MAKAMU Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange
‘Kaburu’ inadaiwa amemuandikia barua pepe, Mwenyekiti wa klabu hiyo, Alhaj
Ismail Aden Rage kumtaarifu kujiuzulu wadhifa huo.
Habari
ambazo JAIZMELALEO imezipata jioni hii zimedai kuwa, Kaburu amemuandikia barua
pepe Rage, ambaye kwa sasa yupo India kwa matibabu ya mgongo kumjulisha uamuzi
wake huo.
Juhudi
za kumpata Kaburu mwenyewe kuzungumzia habari hizo, hazikufanikiwa kutokana na
simu zake zote kutopatikana.
Kaburu
anakuwa kiongozi wa pili wa Kamati ya Utendaji ya Simba kujiuzulu leo, baada ya
awali mchana, Zacharia Hans Poppe aliyekuwa Mjumbe kujiuzulu pia.
Hans
Poppe, aliyekuwa pia Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, alisema kwamba ameamua
kujiuzulu nyadhifa zote hizo kwa sababu kuna mgawanyiko ndani ya uongozi
unaokwamisha maendeleo.
CHANZO: BIN ZUBEIRY