MSANII MAREHEMU OMARY OMARY AZIKWA,VURUGU ZAZUKA MAZISHINI

Baadhi ya wasanii wakibadilishana mawazo kabla ya mazishi.
Waombolezaji akina mama.


Dully Syaks (katikati) akiwa na mapacha Sunche na Kapeto.


Baadhi ya wanamuziki wa kizazi kipya.


Mlevi nmmoja akicheza mbele ya waombolezaji.
Mwili wa marehemu ukisaliwa nyumbani kabla ya kupelekwa makaburini.


Umati ukiwa tayari kwenda makaburini.
Vurugu zikiendelea wakati wa kwenda kuzika.

Vijana waliosababisha vurugu wakisukumana.


Wabeba jeneza wakiwa wanatembea kwa magoti.
MWANAMUZIKI mkongwe wa miondoko ya  mnanda, Omar Omar Mfungilo,  ambaye alifariki usiku wa kuamkia jana ( Jumatatu) nyumbani kwao Temeke-Mkoroshini amezikwa leo katika makaburi ya karibu na nyumbani kwao.
Mazishi hayo ambayo yalihudhuriwa na  watu wengi,  yalitawaliwa na vurugu ambazo zilisababisha baadhi ya waombolezaji kuporwa vitu vyao kama simu, pesa, saa na vitu vingine.
Wakati wa kwenda kumzika, vijana waliojiita ‘kikosi kazi cha mazishi’ waling’ang’ania jeneza lililobeba mwili wa marehemu na kulipeleka wao makaburini huku baadhi  yao wakifanya vitendo vya uporaji njiani wakati wa kwenda kumzika.
                                                        (PICHA/HABARI NA ISSA MNALLY, GPL)
 
© 2012. Design by Ernest James Siwigo Chambasi - Supported By John James Chambasi And Maganza Family