NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI MH PHILIP MULUGO AJA NA MAPYA KATIKA ALAMA MPYA ZA MITIHANI

Naibu waziri Philiph Mulugo
Elimu ya Tanzania iliingia kwenye headlines siku kadhaa zilizopita baada ya kutangazwa kwamba hakutakua na division zero na badala yake kutakua na division five kwa Wanafunzi wanaomaliza elimu ya sekondari.
November 4 2013 Naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Philiph Mulugo ameongea na XXL ya Clouds FM na kusema ‘taarifa zilizotolewa awali zilikosewa kidogo kutokana na mkanganyiko sababu ishu ilikua bado iko kwenye mjadala lakini nataka nikuhakikishie kwamba kutakua na division 1, 2, 3, 4 na kutakua na division zero kama kawaida, haijaondolewa’
‘kinachofanyika tu hapa ni zile point kutanuka baada ya kutoa yale madaraja zile alama kurundikana sehemu moja, tumezihamisha angalau alama zipishane alama 10 mpaka 15 kwa hiyo F itakua ni 0-19 na daraja jingine lililoongezeka pale ni E ambalo 20-29 alafu daraja la D kutakua alama 30 -39, C ni 40 mpaka 49, B ni 50 mpaka 59, B+ ni 60 – 74 alafu A ni 75 mpaka 100′ – 

Naibu waziri Philiph Mulugo
‘Nimeona wadau wengi wanacomment kwenye vyombo vya habari na kwenye mtandao kwamba tumeshusha viwango vya ufaulu, hatujashusha ufaulu ila tumesema tuyaweke haya madaraja kama ni ngazi, swala sio Wanafunzi wote waende form IV lakini kuna vyuo vingine watu wanaweza kwenda kuchukua ujuzi mwingine wa kujishughulisha ila tuwatambue kwamba wamepata alama hizi hapa, anaepata F ambae ni 0-19 ajitambue kwamba hata cheti hawezi kupata, watakaopata cheti ni E na D lakini hawatokua na uwezo wa neno kwamba amepata au amefaulu japo watakua wanaekewa alama zao’ – Philiph Mulugo

Kwa kumalizia Mulugo anasema ‘zamani kulikua kuna A, B, C, D, F lakini sasa kuna A, B+,B, C, D, E na F ukijumlisha zile point zote unakuta mpaka mwishoni kabisa mtu ambae amepata F zote 7 katika masomo ya baraza la mitihani anakua na alama 49 ambayo tunasema huyu kapata 0 division ambayo ndio ilileta mkanganyiko kwa Watanzania na kusema ndio imeitwa division 5, hapana itaendelea kuitwa bado division zero hivyohivyo.
 
© 2012. Design by Ernest James Siwigo Chambasi - Supported By John James Chambasi And Maganza Family