HIVI NDIVYO LADY JAY DEE A.K.A ANACONDA ALIVYOITIKISA NA KUIJAZA NYUMBANI LOUNGE JANA



Mwanadada Judith Mbibo aka Lady Jaydee usiku wa kuamkia Jumamosi ya June 15 amefanikiwa kuweka historia kwenye muziki wa Tanzania kwa kulijaza eneo zima la Nyumbani Lounge alipokuwa akifanya show yake ya kuadhimisha miaka 13 tangu aanze muziki.
 
Hii imedhihirisha kuwa majina anayojiita mwanadada huyu ni ya halali kabisa na yanamfaa kwani tafauti na watu walivyodhan palijaa watu hadi wakaanza kubebana ama kwa hakika huyu ni komando,anaconda hebu anagalia picha mdau utakubaliana na mimi.. PICHA KWA HISANI YA BONGO 5

 Wadau mbali mbali wa muziki hapa nchini wapo ndani ya ukumbi huu kusuhudia show hii ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu na wapenzi wa muziki.
 Ndani ni nyomi la hatari,lakini nje nako watu bado wanataka kuingia huku wengi wao wakisema kuwa "hata kama hakuna siti,sie tuko radhi kusimama ilimradi tumsapoti Dada yetu."


 Foleni bado ni ndefu na watu bado wanazidi kuingia ukumbini hapa hivi sasa.

Katika show hiyo, Lady Jaydee amesindikizwa na wasanii mbalimbali wakiwemo Juma Nature, Sugu, Profesa Jay, Wakazi, Grace Matata na wengine. Pia Jaydee ameitumia siku hiyo kuzindua albam yake mpya, Nothing But The Truth na kusherehekea siku yake ya kuzaliwa. Hizi ni picha za show hiyo.
DSC_4279


DSC_4285
DSC_4288

DSC_4291
DSC_4299
DSC_4300


DSC_4466
DSC_4261
 
© 2012. Design by Ernest James Siwigo Chambasi - Supported By John James Chambasi And Maganza Family