![]() |
| WACHEZAJI wawili wa Tanzania wamechaguliwa miongoni mwa 50
waliofanyiwa majaribio Uganda ili kuingia katika kituo cha kuendeleza
vipaji kilichoko Doha nchini Qatar kupitia mpango wa kukuza vipaji wa
Aspire Football Dream. Abdulrasul Bitebo (15) ambaye ni mshambuliaji kutoka Kituo cha Uwanja wa Karume, na Martin Tangazi (14) ambaye ni beki kutoka Kituo cha Ukonga, wamechaguliwa kutoka Tanzania kuingia katika kituo ambapo watakaa kwa mwezi mmoja kabla ya kusaini mkataba rasmi wa kuendelezwa. Kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), wachezaji wengine walikuwa wakitoka nchi za Uganda na Kenya. Mchezaji mwingine aliyefuzu katika nafasi tatu zilizokuwepo ni kutoka Kenya. Mpango wa Aspire Football Dream unafadhiliwa na Mtoto wa Mfalme wa Qatar katika nchi 16 duniani, na kwa nchini, uko chini ya Idara ya Ufundi ya TFF. TFF ina jumla ya vituo 14 vya kuendeleza vipaji kupitia mpango huo wa Aspire Football Dream. Vituo hivyo ni Karume, Kigamboni, Tandika, Kawe, Ukonga, Kitunda, Mbagala, Magomeni, Makongo, na Tabata vya mkoani Dar es Salaam, Bagamoyo kilichopo mkoani Pwani, Morogoro, Arusha na Moshi mkoani Kilimanjaro. Kituo kingine cha kuendeleza vipaji cha Aspire kipo Dakar nchini Senegal. |
Habari kubwa Magazetini Kenya leo March 3, 2025
8 months ago

