Mhudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa mjini
Singida ambaye jina lake halikuweza kutambuliwa mara moja, akiliweka
sawa jeneza baada ya kufanyiwa ukarabati baada ya kubomolewa na
majambazi na kulisachi. (Picha na Nathaniel Limu).
---
Akifafanua zaidi, amesema kwa upande
wake yeye ameporwa shilingi milioni mbili ambazo zilikuwa kwa ajili ya
kugharamia msafara huo, jumla ya shilingi milioni 8.8 ambazo zilichangwa
na wanafunzi kama rambi rambi kwa mwenzao, na shilingi milioni tisa
ambazo wasindikizaji walikuwa nazo zikiwa ni posho.
“Pia tumeporwa simu zetu zote za mikononi, viatu, laptop na mabegi yote ya nguo zetu”amesema.
Makaranga ambaye amesema anafanya
kazi za kiutawala katika chuo cha SUA, amewataja walioumizwa zaidi ni
pamoja nay eye, dereva Malipula na kiongozi wa wanafunzsi Idd Idd na
kutibiwa katika hospitali ya mkoa na kuruhusiwa.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya
Singida Mwalimu Queen Mlozi, ambaye aliwasiliana na uongozi wa SUA
Morogoro kwa ajili ya shughuli ya kutuma gari jingine na ukarabati wa
jeneza, amesema kuwa kwa ushirikiano wa jeshi la polisi na kamati ya
ulinzi na usalama, watahakikisha watu waliofanya unyama huo, wanakamatwa
mapema iwezekanavyo ili waweze kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.
SOURCE:http://kajunason.blogspot.com/ |