WANACHAMA wa klabu ya Simba ya
jijini Dar es Salaam leo wamefanikiwa kufanya mkutano wao ambao
umeung'oa uongozi uliokuwa chini ya Mwenyekiti wake Aden Ismail Rage.
Mkutano huo licha ya kutokuwa
na baraka ya uongozi wa sasa wa Simba, umefanyika katika Ukumbi wa
Hoteli ya Star Light iliyopo Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Wanachama takribani 506
walihudhuria mkutano huo ambao umemalizika kwa wanachama hao kukubaliana
kuuondoa madarakani uongozi wa Rage ambapo sasa klabu hiyo itaongozwa
na Zacharia Hans Pope pamoja na Rahma Al Kharusi 'Malkia wa Nyuki'
waliochaguliwa kama viongozi wa muda mpaka hapo watakapopatikana
viongozi wapya. |