Rais
mpya wa Madagascar Hery Rajaonarimampianina akiapishwa rasmi rais wa
nchi hiyo mjini Antananarivo kufuatia ushindi mkubwa alioupata katika
uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo mwezi Desemba 2013.
Rais
mpya wa Madagascar Hery Rajaonarimampianina akisani kiapo chake tayari
kuanza kazi ya kuwatumikia wananchi wa Madagascar mbele ya Jaji Mkuu wan
chi hiyo Jean –Michael Rasolonjatovo (kushoto) wakati wa sherehe za
kumuapisha rais huyo zilizofanyika mjini Antananarivo.
Rais
mpya wa Madagascar Hery Rajaonarimampianina akizungumza na wananchi wa
Madagascar waliofurika ndani ya uwanja wa Antananarivo mara baada ya
kuapishwa kuwa rais mpya wa nchi hiyo mjini.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe
akimuwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika sherehe za kumuapisha rais
mpya wa Madagascar akiwa kwenye jukwaa kuu pamoja na viongozi wengine wa
nchi za Afrika waliohudhuria sherehe hizo mjini Antananarivo.Wengine
wanaoonekana kutoka kulia ni Rais mstaafu wa Msumbiji Joachim Chisano,
Rais wa Zambia Ipikefunye Pohamba na aliyekuwa rais wa Madagascar Andry
Raojolina.
Viongozi
mbalimbali na wanachi waliohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais mpya
wa Madagascar Hery Rajaonarimampianina mjini Antananarivo.
Gwaride maalum la jeshi la Madagascar wakati wa sherehe za kuapishwa kwa rais mpya wa nchi hiyo Hery Rajaonarimampianina.
Rais mpya wa Madagascar Hery Rajaonarimampianina akikagua gwaride la majeshi ya Madagascar baada ya kuapishwa.
Rais mpya wa Madagascar Hery Rajaonarimampianina akiwasili Ikulu ya nchi hiyo mjini Antananarivo. Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.
======== ======== ========









