TIZAMA VIONGOZI MBALIMBALI WA NCHI WALIVYOMUENZI WAZIRI MKUU WA ZAMANI MAREHEMU SOKOINE

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (mwenye tracksuti ya bluu),Waziri wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo,Dkt. Fenela Mukangala (wa tano kulia) na Mbunge wa Jimbo la Simanjiro,Mh. Christopher Ole Sendeka,wakishiriki katika matembezi ya nusu kilomita ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 29 tangu kufariki kwa Waziri Mkuu wa zamani,Marehemu Edward Moringe Sokoine,yaliyofanyika leo huko Kijijini kwao Monduli Juu,Mkoani Arusha.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiweka shada la Maua kwenye Kaburi la Waziri Mkuu wa zamani,Marehemu Edward Moringe Sokoine,aliefariki miaka 29 iliyopita siku kama ya leo.
Waziri wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo,Dkt. Fenela Mukangala akiweka shada la Maua kwenye Kaburi la Waziri Mkuu wa zamani,Marehemu Edward Moringe Sokoine.
Wake wa Waziri Mkuu wa zamani,Marehemu Edward Moringe Sokoine wakiweka shada la Maua juu ya kaburi la Mume wao.
Mbunge wa Jimbo la Arusha,Mh. Godbress Lema akishiriki mbio za kumuenzi Waziri Mkuu wa zamani,Marehemu Edward Moringe Sokoine zilizofanyika kijijini kwake Monduni Juu,Mkoani Arusha leo.
Baadhi ya vijana wa jamii ya Kimasai wakikimbia mbio fupi za kumuenzi Waziri Mkuu wa zamani,Marehemu Edward Moringe Sokoine,kijijini kwake Monduli Juu,Mkoani Arusha.
 
© 2012. Design by Ernest James Siwigo Chambasi - Supported By John James Chambasi And Maganza Family